Kilimo mseto (Agroforest) ni kilimo kigeni katika jamii nyingi ya wakulima wa kitanzania ambacho ni mchanganyiko wa mazao ya cha kula na mazao ya mistu ambayo ni rafiki na mazingira, kama vile Ndege chai, chapabunduki (casualina Equistifolia), sedelela, kaya n.k lakini baadhi ya miti ambayo sirafiki na mazingira kama vile mikaratusi (seregena haifai katika kilimo mseto (agroforest).
Ndg Stephen Wambura mkazi wa kijiji cha Gamasara ni miongoni mwa wakulima wa chache ambao wanajihusisha na kilimo mseto.
Ndg wambura anaendelea kusema kuwa anapata faida kubwa sana kutokana na kilimo hiki ambacho hakijazoeleka katika jamii nyingi za kitanzania kwani hutumia eneo lake dogo alilonalo kuzalisha mazao ya chakula na mazao na mbao huku akiendelea kurutubisha shamba kutokana na mboji itokanayo na zao la mistu lililoko shambani kwake.
Mwisho Ndg Stephan Wambura anatoa ushauri kwa jamii na wakulima kwa ujumla watumie njia ya kilimo mseto kwa kupata faida maradufu katika maeneo yao finyu.
Picha Juu: Ndg Stephen Wambu wa pili kulia (mwenye kofia nyeupe) akiwatembeza wanachama kutoka shirika la TAECA na wataalamu kutoka shirika la Vi Agroforest Musoma –Tanzania na kujionea namna anavyoendesha kilimo mseto katika shamba lake.
0 comments :
Post a Comment