Shirika limefanikiwa kuanzisha club ya mazingira ijulikanayo kama mali hai club katika shule ya sekondari Nyamwaga. Wanachama katika club hii ndio wenye wajibu wa kutunza na kusimamia mazingira katika shule yao.
Shirika litawajibika katika kutoa semina utunzaji wa mazingira kwa wanachama wa mali hai club katika shule ya sekondari Nyamwaga.
Picha: Wanachama wa shirika la TAECA wakishirikiana na wanafunzi wa mali Hai club kupanda miche ya
miti katika maeneo ya shule ya Nyamwaga Hill Sekondari .
Shirika limefanikiwa kuandaa na kuendesha semina ya siku tatu ya namna bora ya ufugaji nyuki na uvunaji wa mazao yatokanayo na nyuki kwa wanacha wa shirika la TAECA na washiriki wengine kutoka kikundi cha ufugaji nyuki cha wazee wa mila Bwirege na kikundi cha ufugaji nyuki kutoka kijiji cha Nyarero.
jinsi gani shule yangu inaweza kujiunga na kikundi cha utunzaji wa mazingira
ReplyDelete