TARIME AGRICULTURAL AND ENVIRONMENTAL CONSERVATION ASSOCIATION

Shirika la Tarime Agricultural and Environmental conservation Association (TAECA) ni shirika lisilo la kiserikali (NGO) lililoanzishwa mwaka 2014 na kupata usajili kamili tarehe 14 mwezi 04 mwaka 2015. na kupewa namba ya usajili 00NGO/0007915.

Lengo kuu la shirika ni kuunganisha Nguvu ya pamoja katika kutoa elimu juu ya kanuni bora za kilimo, ufugaji, Elimu jamiii na ujasirialimali kwa lengo la kuinua uchumi katika jamii ya kitanzania.

Eneo la utendaji kazi la shirika la TAECA ni katika eneo lote la Tanzania Brara na ofisi ndogo zitafunguliwa kila sehemu ambapo shirika litakuwa na mradi.

DIRA YA SHIRIKA (VISION)
Kuwa na jamii inayoendesha shughuli za kilimo/ufugaji endelevu kwa kufuata misingi   bora ya kilimo na ufugaji kwa lengo la kukuza uchumi wa kizazi cha sasa na kijacho.

DHAMIRA YA SHIRIKA (MISSION)
Kuiwezesha jamii, sekta binafsi na wadau wengine kushiriki katika kuinua kilimo, ufugaji na utunzaji wa mazingira kwa kutumia mbinu shirikishi jamii ili kuleta tija na uchumi imara katika jamii ifikapo mwaka 2050.

About TAECA.TZ

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment